Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Mipango

TUME YA TAIFA YA MIPANGO YAKAMILISHA MAFUNZO YA MWONGOZO WA NDPAG  KWA WATENDAJI 500
06 Aug, 2026
TUME YA TAIFA YA MIPANGO YAKAMILISHA MAFUNZO YA MWONGOZO WA NDPAG  KWA WATENDAJI 500


Tume ya Taifa ya Mipango imekamilisha utoaji wa mafunzo ya Mwongozo wa Kitaifa wa Uidhinishaji wa Miradi ya Maendeleo (NDPAG) Kwa Maafisa Mipango na Wakuu wa Idara/Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathimini 500 kutoka nchini  nzima 

‎Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Meneja Miradi ya kitaifa kutoka  Tume ya Taifa ya Mipango, Bw. Royal John Lyanga, amesema  mafunzo hayo yalilenga  kuwajengea uwezo maafisa hao ili waondokane  na kufanya kazi kwa mazoea kuelekea Julai Mosi ambapo  utekelezaji wa  Dira 2050 utaanza rasmi.

‎Ameeleza kuwa Miradi yote ya kitaifa kwenye mikoa, wilaya na halmashauri kuanzia sasa itaandaliwa kitaalamu kwa kufuata mwongozo huo na kuwasilishwa kwenye ngazi husika kupitia mfumo wa e-Delivery.

‎Mfumo wa e-Delivery utazingatia viwango vya ubora wa maandiko ya miradi, mfumo mzima wa ufuatiliaji na tathimini pamoja na maandalizi bora ya miradi. 

‎Tume ya Taifa ya Mipango imeendelea kutoa mafunzo Kwa watendaji wa kada mbalimbali nchini kwa lengo la kujenga uelewa wa miongozo na mifumo mbalimbali itakayotumika kuanzia  Julai Mosi katika utekelezaji wa Dira 2050.