Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Mipango (PC)

Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano

Lengo

Kutoa utaalamu na huduma za TEHAMA kwa Tume.

Kitengo kitatekeleza majukumu yafuatayo:

  1. Kuandaa mifumo ya ufuatiliaji na utoaji taarifa.
  2. Kuwezesha matumzi ya TEHAMA katika utendaji kazi.
  3. Kuanzisha na kusimamia miundombinu ya mtandao wa mawasiliano ya Tume.
  4. Kusimamia na kuhuisha tovuti ya Tume.
  5. Kutoa huduma za kiufundi za TEHAMA kwa Tume.
  6. Kusanifu na kusimamia usalama wa mfumo.
  7. Kuwezesha kufanyika kwa shughuli za Serikali mtandao na Biashara ya kielektroniki.
  8. Kufanya tafiti na kupendekeza maeneo ya kutumia TEHAMA kama chombo cha kuboresha utoaji wa huduma katika Tume;

Kitengo hiki kitaongozwa na Meneja.