Utangulizi
Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), ilianzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Tume ya Taifa ya Mipango, Sura Namba 127, ikiwa na majukumu mbalimbali yakiwemo kuratibu usimamizi wa uchumi, kupanga mipango ya maendeleo, na kutekeleza mipango ya maendeleo iliyoidhinishwa.
Tume inafanya kazi chini ya Kamisheni na inaongozwa na Rais, ambapo inatumika kama chombo kikuu cha ushauri kwa Serikali kuhusu masuala yanayohusiana na usimamizi wa uchumi na mipango ya maendeleo ya Taifa.
Pamoja na majukumu mengine, NPC imepewa jukumu la kuandaa mipango ya maendeleo ya Taifa ya muda mrefu, kati na mfupi. Vilevile, Tume ina jukumu la kufuatilia utekelezaji wa mipango hiyo ya maendeleo, ikiwemo miradi mikubwa na ya kimkakati, kwa lengo la kuchochea maendeleo ya Taifa. Aidha, Tume inawajibika kuandaa Dira ya Taifa ya Maendeleo ambayo hutumika kama mwongozo mkuu katika kupanga maendeleo ya nchi.