Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Fred Msemwa, pamoja na wajumbe wa Menejimenti ya NPC wamekutana na Tume ya Maboresho ya Sheria inayoongozwa na Katibu Mtendaji Bw. George Mandepo na kujadili maboresho ya sheria yatakayowezesha utekelezaji wa Dira 2050, ikiwa ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais yaliyotolewa wakati wa uzinduzi wa Dira hiyo.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango(NPC), Dkt. Fred Msemwa, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera, kuhusu masuala ya maendeleo ya Taifa. Mazungumzo hayo yamefanyika leo, tarehe 26 Januari 2026, katika Ofisi za NPC Dodoma
KAULI MBIU:
Kuileta Dunia Pamoja Kupitia Dira ya Mwaka 2050: Kutumia Takwimu za Idadi ya Watu na Mbinu Bunifu za Mipango Endelevu na Ustahimilivu
Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango(NPC), Dkt. Fred Msemwa (Kushoto) akiwa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Shigeki Komatsubara baada ya mazungumzo yaliyofanyika Ofisi za NPC Dodoma. Desemba 11, 2025.
Naibu Katibu Mkuu, UTUMISHI, Xavier Daudi (wa kwanza kushoto mbele) akifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Meneja wa Mawasiliano Serikalini, Titus Kaguo wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), juu ya wajibu na majukumu ya NPC, leo 13.10.2025 ofisi ya UTUMISHI, Mtumba, Dodoma.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Fred Msemwa atembelea vituo Television na Radio vya IPP Media jijini Dar es Salaam, ziara iliyolenga kuhamasisha vyombo vya habari nchini kuongeza juhudi katika utoaji wa elimu juu ya utekekezaji wa DIRA 2050.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Fred Msemwa akiwasilisha mada juu ya Utekelezaji wa 2050 katika Mkutano Mkuu wa 27 wa Baraza la Habari Tanzania( leo 25.9.2025) jijini Dar es Salaam
Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Fred Msemwa, akiwasilisha mada juu ya Utekelezaji wa DIRA 2050 katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wahandisi, leo tarehe 26 Septemba 2025, ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango(NPC), Dkt. Fred Msemwa (kushoto), akipokea Mkakati wa Muda wa Kati wa Ukusanyaji wa Mapato wa Miaka Mitatu (Medium Term Revenue Strategy) kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba katika hafla ya uzinduzi wa mkakati huo uliofanyika katika ukumbi wa Kambarage, Treasury Square, jijini Dodoma (leo). Mkakati huo unatarajiwa kutekelezwa kuanzia mwaka wa fedha 2025/2026 hadi 2027/2028. Uzibduzi wa Mkakati huo umekwenda sambamba na kuzinduliwa kwa Kamati za Usimamizi na Utekelezaji wa Mkakati huo.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Fred Msemwa (kulia) akimkaribisha Mkurugenzi mpya wa Maendeleo wa Ubalozi wa Uingereza nchini, Bi. Anna Wilson alivyotembelea ofisi za NPC jijini Dodoma.