Naibu Katibu Mkuu, UTUMISHI, Xavier Daudi (wa kwanza kushoto mbele) akifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Meneja wa Mawasiliano Serikalini, Titus Kaguo wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), juu ya wajibu na majukumu ya NPC, leo 13.10.2025 ofisi ya UTUMISHI, Mtumba, Dodoma.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Fred Msemwa atembelea vituo Television na Radio vya IPP Media jijini Dar es Salaam, ziara iliyolenga kuhamasisha vyombo vya habari nchini kuongeza juhudi katika utoaji wa elimu juu ya utekekezaji wa DIRA 2050.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Fred Msemwa akiwasilisha mada juu ya Utekelezaji wa 2050 katika Mkutano Mkuu wa 27 wa Baraza la Habari Tanzania( leo 25.9.2025) jijini Dar es Salaam
Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Fred Msemwa, akiwasilisha mada juu ya Utekelezaji wa DIRA 2050 katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wahandisi, leo tarehe 26 Septemba 2025, ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango(NPC), Dkt. Fred Msemwa (kushoto), akipokea Mkakati wa Muda wa Kati wa Ukusanyaji wa Mapato wa Miaka Mitatu (Medium Term Revenue Strategy) kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba katika hafla ya uzinduzi wa mkakati huo uliofanyika katika ukumbi wa Kambarage, Treasury Square, jijini Dodoma (leo). Mkakati huo unatarajiwa kutekelezwa kuanzia mwaka wa fedha 2025/2026 hadi 2027/2028. Uzibduzi wa Mkakati huo umekwenda sambamba na kuzinduliwa kwa Kamati za Usimamizi na Utekelezaji wa Mkakati huo.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Fred Msemwa (kulia) akimkaribisha Mkurugenzi mpya wa Maendeleo wa Ubalozi wa Uingereza nchini, Bi. Anna Wilson alivyotembelea ofisi za NPC jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango(NPC) Dkt. Mursali Milanzi (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa NPC, Wafanyakazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu(UNFPA) na Waandishi wa Habari wakati wa Semina Elekezi juu ya kubobea )kwenye uandishi wa majukumu ya NPC, ikiwemo DIRA 2050,, iliyofanyika jijini Dar es Salaam, hivi karibuni
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, akiagana na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Fred Msemwa, mara baada ya kufunga Mkutano wa Mashirika ya Umma (SOEs Conference), leo Agosti 26, 2025, Jijini Arusha.
Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango (NPC), Dkt. Blandina Kilama, tarehe 5 Agosti 2025, aliongoza Kongamano la Wadau wa Kilimo jijini Dodoma kujadili mchango wa sekta hiyo katika utekelezaji wa DIRA 2050, kuelekea siku ya kilele cha Maonesho ya Nane Nane, likiwa na lengo la kuongeza tija, ushindani na ushirikiano wa wadau wote.
NPC Yatangaza Kukamilika kwa Mpango wa Miaka Mitano Novemba; Serikali Yasisitiza Maboresho ya Sera na Utumishi kwa Utekelezaji wa DIRA 2050