Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Taifa ya Mipango

Kitengo cha Fedha na Uhasibu

Lengo

Kutoa huduma bora za usimamizi wa fedha na uhasibu.

Kitengo kitatekeleza majukumu yafuatayo:

  1. Kuandaa Taarifa za Fedha za Robo Mwaka, Nusu Mwaka na Mwaka.
  2. Kukagua Vocha za Malipo na nyaraka zinazoambatana nazo ili kuzingatia Sheria za Usimamizi wa Fedha.
  3. Kuratibu na kujibu hoja za ukaguzi zinazoibuliwa.
  4. Kushughulikia malipo ya fedha taslimu na kutunza nyaraka za fedha.
  5. Kuandaa malipo ya mishahara na kuhakikisha makato yote ya kisheria yanatumwa kwa wakati kama inavyoelekezwa.
  6. Kuandaa, kufanya malipo na kufuatilia matumizi.

Kitengo hiki kitaongozwa na Mhasibu Mkuu.