Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi Kida kwenye picha ya pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Prof. William Anangisye baada ya mjadala wa maendeleo ya nchi za bara la Afrika kujitegemea kiuchumi uliofanyika katika kongamano la 17 la Kigoda cha Kiprofesa cha Mwalimu Julius Nyerere.
Katika Kongamano hilo Dkt Kida alitoa hotuba ya utangulizi ambapo amesema ili kufanikisha mipango mbalimbali ya maendeleo kunahitaji kuwa na amani, utulivu na utawala bora, hivyo alitoa wito kwa Afrika kuimarisha utawala bora, kuheshimu haki za binadamu na utawala wa sheria ili kuwa na bara la lenye amani na utulivu.
Katibu Mkuu (Mipango) na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi Mbaga Kida, ameshiriki katika kikao kazi maalum kilichojadili changamoto za upatikanaji wa mbolea duniani na mikakati iliyowekwa na Tanzania kuwawezesha wakulima. Majadiliano hayo yamefanyika katika Chuo Kikuu cha George Washington nchini Marekani pembezoni mwa mfululizo wa Vikao vya Kipupwe (Spring Meetings) vinavyoendelea jijini Washington DC.
Katibu Mkuu Mipango na Katibu Mtendaji Tume ya Taifa ya Mipango Dkt Tausi Kida, ameshiriki katika kikao cha ngazi ya wataalamu kutoka Tanzania na ujumbe wa Benki ya Dunia, ambacho kimejadili miradi ya kipaumbele ya Serikali katika sekta mbalimbali itakayopewa ufadhili wa Benki ya Dunia kupitia Mzunguko wa 21 wa IDA (IDA-21 Cycle).
Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Blandina Kilama leo amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Ubalozi wa Urusi jijini Dar es Salaam. Mazungumzo hayo yalihusu maandalizi ya Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Biashara kati ya Tanzania na Urusi, unaotarajiwa kufanyika mwezi Mei 2026 hapa nchini.
Tume ya Taifa ya Mipango imekutana na kufanya majadiliano na washirika wa maendeleo leo Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa kimaendeleo.
Tume ya Taifa ya Mipango imekutana na kufanya majadiliano na washirika wa maendeleo leo Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa kimaendeleo.
Katibu Mkuu-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt Tausi M. Kida ametoa wito kwa watendaji wa Tume hiyo kufanya kazi kwa weledi, ubunifu na ushirikiano ili kuishi dhana ya kufanya kazi isivyokawaida ili kuyafikia matarajio ya Taifa jumuishi, lenye ustawi, haki na linalojitegemea.
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais-Mipango na Katibu Mtendaji Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt Tausi Kida amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Indonesia nchini, Mhe. Tri Yogo Jatmiko Avetisyan leo jijini Dar es Salaam. Mazungumzo baina ya viongozi hao yameangazia Mipango ya Maendeleo hususani katika kuendeleza miradi mbalimbali katika sekta ya Kilimo na ufugaji.
Katibu Mkuu (Mipango) na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi M. Kida akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Watendaji wa Tume, na baadhi ya Watafiti kutoka katika taasisi za tafiti nchini, wakati wa kikao kazi baina ya Tume na Taasisi za Tafiti nchini kinachofanyika kwa mud awa siku mbili katika jengo la Mkemia Mkuu wa Serikali Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, amekutana na kufanya mazungumzo na Bi. Julia Kronberg, Mkuu wa Ushirikiano wa Maendeleo Tanzania na Afrika Mashariki kwenye Ubalozi wa Ujerumani hapa nchini, leo Machi 12, 2026 jijini Dodoma.