Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. James Kinyasi Millya (Mb.) (wa nne kutoka kushoto), Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi Mbaga Kida (wa tatu kutoka kushoto), na Bw. Shigeki Komatsubara, Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini Tanzania (wa nne kutoka kulia), pamoja na viongozi mbalimbali na wadau wa maendeleo, wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Ubunifu Tanzania, leo Agosti 31, 2026, jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi Mbaga Kida, akizungumza na Bi. Akoth O. Kidew (miaka 11), Mwanzilishi na Kiongozi Mkuu wa Shirika la Small Hands, Big Change, mara baada ya ufunguzi wa Wiki ya Ubunifu Tanzania 2026, inayofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 31 Agosti hadi 04 Septemba 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, amesema Serikali inalenga kuhakikisha ukuaji wa uchumi wa Tanzania unaendana na ongezeko la ajira na kipato kwa wananchi, akibainisha kuwa azma hiyo ni sehemu ya juhudi za kujenga uchumi jumuishi unaowanufaisha Watanzania. Mhe. Mkumbo ameyasema hayo, Agosti 31, 2026, jijini Dar es Salaam, wakati akifungua Wiki ya Ubunifu Tanzania 2026, iliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Tume ya Taifa ya Mipango, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na wadau mbalimbali.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, leo Agost 20, 2026 amefanya mazungumzo na Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Bw. Eliakimu Maswi, kuhusu ufungamanishaji wa Ajenda ya Kitaifa ya Mageuzi ya Kijamii na Maendeleo ya Mtaji Watu katika Kufikia Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na Dira 2050.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, akiwasilisha taarifa kuhusu mikakati ya kuhakikisha sera, sheria na kanuni zinaendana na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Bungeni jijini Dodoma, Agosti 17, 2026.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, amesema ushirikiano kati ya Serikali, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Tanzania na wadau mbalimbali ni muhimu katika kugeuza ubunifu, teknolojia na utafiti kuwa chachu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Unaweza kujisajili sasa kupitia https://summitpoint.co.tz/events/iwtz-2026
Tume ya Taifa ya Mipango imeshiriki katika maadhimisho ya wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu 2026 yanayoendelea jijini Tanga yakiongozwa na kauli mbiu imesemayo “Elimu, Ujuzi na Ubunifu njia ya kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050”.
PLANNERS' CONFERENCE 2026 | AICC - ARUSHA | FOR REGISTRATION - SCAN QR CODE
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi Kida ameongoza kikao cha Makatibu Wakuu kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. Jim Yonazi kilicholenga kujadili utendaji wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka -BRT leo 04 Agosti, 2026 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Nyenzo za Utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 03 Agosti, 2026.