Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, leo Agost 20, 2026 amefanya mazungumzo na Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Bw. Eliakimu Maswi, kuhusu ufungamanishaji wa Ajenda ya Kitaifa ya Mageuzi ya Kijamii na Maendeleo ya Mtaji Watu katika Kufikia Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na Dira 2050.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, akiwasilisha taarifa kuhusu mikakati ya kuhakikisha sera, sheria na kanuni zinaendana na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Bungeni jijini Dodoma, Agosti 17, 2026.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, amesema ushirikiano kati ya Serikali, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Tanzania na wadau mbalimbali ni muhimu katika kugeuza ubunifu, teknolojia na utafiti kuwa chachu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Unaweza kujisajili sasa kupitia https://summitpoint.co.tz/events/iwtz-2026
Tume ya Taifa ya Mipango imeshiriki katika maadhimisho ya wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu 2026 yanayoendelea jijini Tanga yakiongozwa na kauli mbiu imesemayo “Elimu, Ujuzi na Ubunifu njia ya kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050”.
PLANNERS' CONFERENCE 2026 | AICC - ARUSHA | FOR REGISTRATION - SCAN QR CODE
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi Kida ameongoza kikao cha Makatibu Wakuu kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. Jim Yonazi kilicholenga kujadili utendaji wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka -BRT leo 04 Agosti, 2026 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Nyenzo za Utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 03 Agosti, 2026.
Tume ya Taifa ya Mipango imeshiriki Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kwa kutoa elimu kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na nafasi yake katika kuendeleza biashara na uwekezaji.
Katika Jukwaa la Ngazi ya Juu la Siasa la Umoja wa Mataifa la Utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu lililofanyika New York, Dkt. Tausi Kida (Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango) ameeleza kuanza rasmi kwa utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (FYDP IV), ikiwa ni hatua ya kwanza ya kutekeleza Dira 2050 iliyozinduliwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mwezi Julai 17, 2025.
Tume ya Taifa ya Mipango imeanza rasmi kutumia mfumo mpya wa Kitaifa wa kusimamia Mipango na Miradi ya Maendeleo wa e-Delivery System kuanzia Julai Mosi 2026