Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi Kida ameongoza kikao cha Makatibu Wakuu kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. Jim Yonazi kilicholenga kujadili utendaji wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka -BRT leo 04 Agosti, 2026 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Nyenzo za Utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 03 Agosti, 2026.
Tume ya Taifa ya Mipango imeshiriki Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kwa kutoa elimu kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na nafasi yake katika kuendeleza biashara na uwekezaji.
Katika Jukwaa la Ngazi ya Juu la Siasa la Umoja wa Mataifa la Utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu lililofanyika New York, Dkt. Tausi Kida (Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango) ameeleza kuanza rasmi kwa utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (FYDP IV), ikiwa ni hatua ya kwanza ya kutekeleza Dira 2050 iliyozinduliwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mwezi Julai 17, 2025.
Tume ya Taifa ya Mipango imeanza rasmi kutumia mfumo mpya wa Kitaifa wa kusimamia Mipango na Miradi ya Maendeleo wa e-Delivery System kuanzia Julai Mosi 2026
Tanzania inatarajiwa kuwasilisha ripoti ya nchi kuhusu
utekelezaji wa Ajenda 2030 ya malengo ya maendeleo endelevu Julai 14, 2026 Jijini New York nchini Marekani kwenye Jukwaa la Ngazi ya Juu la Siasa la Umoja wa Mataifa litakaloanza vikao vyake kuanzia Julai 7-15, 2026, Jijini humo.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais (Mipango) na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi M. Kida, akiwa katika picha na Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications, Bi. Rosalynn Mndolwa-Mworia, jijini Dar es Salaam mara baada ya mazungumzo baina yao yaliyoangazia ushirikiano wa taasisi hizo mbili katika kusukuma mbele ajenda za utekelezaji wa Dira 2050 kupitia mawasiliano ya kimkakati.
Tume ya Taifa ya Mipango imeandaa Mwongozo na Mkakati wa Kitaifa wa ushirikishwaji wa Sekta Binafsi katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya Taifa ikiwemo Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (FYDP IV) katika utekelezaji wa Dira 2050 inayoanza rasmi Julai Mosi 2026
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt Tausi Kida akitoa elimu kwa wananchi mbalimbali juu ya utekelezaji wa Dira 2050 katika maonesho ya wiki ya utumishi wa umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali Park-Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dkt. Tausi Kida, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika Mashariki na Kusini wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bw. Sakphouseth Meng, aliyeambatana na Mratibu wa Programu za IFAD nchini, Bi. Jacqueline Machangu-Motcho.